Alhamisi 20 Machi 2025 - 13:02
Ujumbe wa Ayatollah Subhani kuhusu maadhimisho ya Kumbukizi ya Ujenzi wa Msikiti wa Jamkaran

Ayatollah Subhani alitoa jumbe tofauti katika kuadhimisha miaka 1073 tangia ujenzi wa Msikiti  mtukufu wa Jamkarani kwa amri ya Imaam wa zama (aj).

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, Ayatollah Subhani aliithamini siku ya ujenzi wa Msikiti wa Jamkarani.

Maelezo ya ujumbe wake ni kama ifuatavyo:
Bismillah al-Rahman al-Rahim
Mwezi mtukufu wa Ramadhani, ni mwezi wa kushuka rehema za Mwenyezi Mungu, baraka zisizo hesabika na msamaha wa dhambi.

Kwa mujibu wa nukuhu, Msikiti wa Jamkaran ulijengwa mnamo tareh 17 Ramadhani mwaka 373 Hijria, kwa mwongozo wa Imam Al-Zaman (a.j), na leo hii mahali hapa ni Qabah ya mioyo ya wapenzi wa wilaya na wenye kusubiri kudhihiri kwa alie hoja ya mwisho ya Mwenyezimungu.

Bila shaka, mahali hapa takatifu ni ishara ya muungano wa kina wa waumini na Imam Al-Zaman (a.s), na ni fursa ya kipekee kwa wapenzi wa Imam huyo katika faragha kumuomba Mwenyezi Mungu kwa moyo uliojaa upendo na matumaini, na kutaka kuharakishwa kudhihiri kwake.

Ni uzuri ulioje  katika usiku hu wa Qadr na katika sehemu hii, tuielekeze mikono yetu kwa Mwenyezi Mungu, tukimuomba heshima na utukufu kwa Waislamu wote, kuangamizwa maadui wa Uislamu, na kuondoa uovu wa maadui wa dini.

Ja'far Subhani

Lebo

Maoni yako

You are replying to: .
captcha